button

anim

Tally

advert2

security

Advert

Advert
Advert

babu

babu
leokwetu

mochrispoadver

pub

pub

flashplayer

Sunday, October 5, 2014

Batuli Afunguka Kuhusu Tetesi ya Yeye Kuvunja Uchumba wa Rose Ndauka

Stori: RHODA JOSIAH
MSANII wa filamu Bongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ameshangazwa na madai kuwa, anahusika kuvunjika kwa uchumba wa msanii mwenzake Rose Ndauka na kueleza kuwa hayo ni maneno ya watu wasiomtakia mema.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni kufuatia madai hayo, Batuli alisema hajawahi kuwa na uhusiano wowote na bwana wa Rose (Malick) na kwamba ukaribu wao ni wa kikazi tu.

“Jamani siwezi kutoka na mchumba wa Rose kutokana na kwamba ni mtu ambaye namheshimu sana na tumekuwa tukifanya kazi na Rose bila matatizo yoyote. Hizi taarifa zinanishangaza na najua wanaozieneza hawanitakii mema,” alisema Batuli.